Jibu la Biblia
Mwandishi wa Biblia, Luka, alisema hivi kuhusu masimulizi aliyoandika kuhusu maisha ya Yesu: “
nimefuata kwa uangalifu mambo yote tangu mwanzo kwa usahihi.”—Luka 1:3.
Watu
fulani wanadai kwamba masimulizi ya maisha ya Yesu yaliyoandikwa katika
Vitabu vya Injili, yaani, maandishi ya watu walioishi wakati wake kama
vile Mathayo, Marko, Luka, na Yohana, yalibadilishwa wakati fulani
katika karne ya nne.
Hata
hivyo, sehemu fulani muhimu ya Injili ya Yohana ilipatikana nchini Misri
mwanzoni mwa karne ya 20. Sehemu hiyo inajulikana kama Papyrus Rylands 457 (P52) na imehifadhiwa katika Maktaba ya John Rylands Library, huko Manchester, Uingereza. Ina kitabu cha Yohana 18:31-33, 37, 38 katika Biblia za leo.

No comments:
Post a Comment